Home » » Afunguliwa kesi ya “kuvuruga amani ya umma” kisa soksi zake

Afunguliwa kesi ya “kuvuruga amani ya umma” kisa soksi zake

Unknown | Monday, December 04, 2017 | 0 comments
Polisi nchini India wanasema wamemkamata mwanamume mmoja ambaye uvundo wa soksi zake ulisababisha ugomvi kati yake na abiria wenzake kwenye basi.
Waliambia BBC kwamba wamewasilisha kesi dhidi ya Prakash Kumar, 27, kwa “kuvuruga amani ya umma”.
Kisa hicho kilitokea kwenye basi lililokuwa safarini kuelekea mji mkuu Delhi, baada ya Kumar kuvua viatu vyake na soksi.
Harufu mbaya kutoka kwenye soksi zake ilikuwa mbaya sana kiasi kwamba abiria walimuomba Bw Kumaru kuziweka ndani ya mkoba wake au kuzirusha nje ya basi.
Lakini anadaiwa kukataa hilo, na ugomvi mkali ukazuka.
Abiria kisha walimlazimisha dereva wa basi hilo kuingia kituo cha polisi katika jimbo la Himachal Pradesh, kaskazini mwa India, ambapo malalamishi dhidi yake yaliwasilishwa.
Gazeti la Hindustan Times limemnukuu Bw Kumar akisema kwamba soksi zake hazikuwa na harufu mbaya, na kwamba abiria wenzake waligombana naye “bila sababu”.
Polisi wameambia BBC kwamba mwanamume huyo amepewa dhamana.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG