Home » » Wafanyakazi mkoani njombe wameiomba serikali kuwaongezea watumishi wa umma stahiki ,kupanda madaraja pamoja na mishaara

Wafanyakazi mkoani njombe wameiomba serikali kuwaongezea watumishi wa umma stahiki ,kupanda madaraja pamoja na mishaara

Unknown | Tuesday, May 01, 2018 | 0 comments

Wafanyakazi mkoani njombe wameiomba serikali kuwaongezea watumishi wa umma  mishahara na kulipa malimbikizo ya mishahara kwa wafanya kazi pamoja na kupandishwa madaraja

Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi hii leo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambayo katika mkoa wa njombe yamefanyika wilaya ya makete viwanja vya mabehewani Makete mjini katibu wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania [TUCTA] ambaye pia ni katibu  wa chama cha walimu mkoa wa njombe [CWT] FRANTEN KWAHHISON amesema hali ya  maisha ya mtanzania  imekuwa ikipanda kila siku lakini mishahara ya watumishi imekuwa haiendani na maisha halisi.

Sambamba na hilo wameiomba serikali kupandisha mishahara ya watumishi waliopandishwa vyeo kuanzia mwaka 2016 kwani watumishi hao ni haki yao ya kupandishwa mishahara ili waongeze ufanisi Mzuri wa ufanyaji kazi.

Vyama shirikisho vya  wafanyakazi mkoa wa njombe vimeishukuru serikali ya awamu ya tano kwa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha  standard geurge, kuwarudisha watendaji wa vijiji ambao walikosa sifa kutokana na kutokuwa na vyeti vya kidato cha nne huku wakiipongeza serikali kwa usimamizi mzuri wa uchumi wa nchi.

Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya  wafanyakazi katika mkoa wa njombe alikuwa ni mkuu wa mkoa wa njombe mh CHRISTOPHA OLE SENDEKA katika sherehe hizi amewakirishwa na mkuu wa wilaya ya makete mh VERONIKA KESSY kwa niaba ya mkuu wa mkoa  amesma changamoto zote ambazo watumishi wanakumbana nazo serikali ya awamu ya tano itazishughulikia ikiwemo malimbikizo mbalimbali ya mishara ya watumishi pamoja na fedha ya uhamisho kwa watumishi huku akiwaomba wafanyakazi kuwa wavumilivu maana serikali ya dakta john pombe magufuli ni sikivu itatatua changamoto hizo.

Veronika kessy amewaomba wananchi wa mkoa wa njombe pamoja na wafanya kazi kwa ujumla kutambua kuhusu ugonjwa wa virusi vya  ukimwi [VVU] ambao umekuwa ni janga kubwa katika mkoa wa njombe na amewaomba kwenda vituo vya afya kujitokeza kupima ugonjwa huo.


Maadhimisho hayo yameambatana na kaulimbiu isemayo KUUNGANISHWA KWA MIFUKO YA  HIFADHI YA JAMII KULENGO KUBORESHA MAFAO YA WAFANYA KAZI. 
baadhi ya picha za mei mosi

































Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG