Home » » VIDEO :MBUNGE WA JIMBO LA MAKETE PROF NORMAN ADAMSON SIGARA KING AKONGA NYOYO ZA WANAISAPULANO

VIDEO :MBUNGE WA JIMBO LA MAKETE PROF NORMAN ADAMSON SIGARA KING AKONGA NYOYO ZA WANAISAPULANO

Unknown | Thursday, February 01, 2018 | 0 comments


Mbunge wa jimbo la Makete Prof. Norman Adamson Sigara King amechangia mifuko ya saruji zaidi ya sabini (70)  kwa ajili ya kumalizia jengo la maabara pamoja na mabati mia moja  kwaajili ya kuchangia ujenzi wa madarasa ya Shule ya Secondari ya Isapulano Ambayo kwa sasa imeshaanza Rasmi.

Mh.Sigara ametoa Mchango huo alipo kuwa akiwasilisha hati ya usajili wa shule hiyo kwa wananchi ambao kwa kipindi cha miaka mingi walikuwa wakipata huduma ya shule kwa umbali mrefu hivyo kupelekea gharama za maisha kuwa juu kila siku.

wananchi wa kata ya Isapulano wamesema kuanza kwa shule hiyo kumefuta machozi ya mudamrefu ambapo kwasasa wamehamasika kupeleka watoto wao shule huku wakimshukuru mgunge kwa kushirikiana na halmashauri kufanikisha kufunguliwa kwa shule hiyo

Tazama video hiyo


Mh: Mbunge Prof Sigara akizungumza na wananchi wa Isapulano

Mbunge akiahidi mchango wake huku akisisitiza kauli mbiu yake ya kazi kwanza maneno baadaye
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG