Home » » UNESCO WAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUFANYA UANDISHI WA HABARI WENYE TIJA

UNESCO WAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUFANYA UANDISHI WA HABARI WENYE TIJA

Unknown | Monday, February 12, 2018 | 0 comments

SHIRIKA la umoja wa Kimataifa la Elimu,Sayansi,Mazingira na Utamaduni-UNESCO-Limewataka waandishi wa habari za redio za kijamii nchini kutumia mafunzo ya uandishi wa habari wanayopata ili kufikisha taarifa sahihi na zenye tija kwa jamii inayowazunguka.
Wito huo umetolewa leo mjini Dodoma na Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la UNESCO Dar es salaam  Bi Faith Shayo wakati akiongea na waandishi wa habari zaidi ya 40 wa redio za kijamii nchini wanaomaliza mafunzo yao leo yanayotolewa na shirika hilo katika ukumbi wa wakala wa ujenzi-TBA-.
Bi Shayo amesema redio za kijamii zina nguvu kubwa ya kufikisha ujumbe kwa haraka katika jamii hivyo waandishi wa habari wana jukumu kubwa la kufanya kazi kwa weledi ili kuzisaidia jamii zilizoko pembezoni ili ziweze kufikia malengo ya maendeleo ya millennia.
Sambamba na hayo amewataka waandishi wa habari kuandika habari zenye uzania ili kuondoa migogoro katika jamii ikiwa ni pamoja na kuyafikia makundi maalumu ambayo mara nyingi yamekuwa yakitengwa .
Kwa upande wake Afisa wa mawasiliano wa Tume ya Taifa ya UNESCO(NATCOM) Bi  Cristina ametoa wito kwa waandishi wa habari kutumia vizuri mafunzo ya Tehama ili kuwarahisishia kusambaza habari kwa urahisi katika jamii kulingana na kasi ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.
Semina hiyo ya siku 12 iliyojumuisha waandishi wa habari 49 wa redio za kijamii 24 nchini,imelenga kujifunza namna ya kuandika habari za uchunguzi,kutangaza habari za michezo kwa kuzingatia jinsia ikiwa ni pamoja na kujifunza namna ya ufuatiliaji na tathimini ya taarifa za habari.



 Afisa wa mawasiliano wa Tume ya Taifa ya UNESCO(NATCOM) Bi  Cristina






BI,ROSE MWALONGO
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG