Rais
Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amekiri kufuta kauli yake
iliyodumu kwa takribani miaka 30 kuwa Tanzania ni kichwa cha
mwendawazimu na haitakaa ifanye vizuri kwenye michezo.
Mwinyi
ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali
kati ya Simba SC dhidi ya Gendarmerie ya Djibouti, baada ya mchezo
alisema kiwango cha mpira nchini kwasasa kimekua hivyo anafuta kauli
yake.
''Mchezo
umekuwa mzuri na sasa nafuta lile neno (Tanzania ni kichwa cha
Mwendawazimu anayejifunza kunyoa atunyoe sisi) lakini sasa sisi ndio
vinyozi'', alisema.
Katika
mchezo wa jana Simba SC iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 hivyo kujiweka
vizuri kwenye mchezo wake wa marudiano huko Djibouti. Yanga pia
ilishinda dhidi ya St. Louis ya Shelisheli.
Yanga
inayocheza klabu bingwa Africa itasafiri kwenda Shelisheli kwaajili ya
mchezo wake wa marudiano Februari 20 huku Simba inayoshiriki Kombe la
Shirikisho nayo itasafiri kuelekea Djibouti kwaajili ya mchezo wa
Februari 20 au 21.
0 comments:
Post a Comment