Home » » MKUU WA SHULE AKIRI KUTUMIA VIBAYA FEDHA ZA SHULE MAKETE

MKUU WA SHULE AKIRI KUTUMIA VIBAYA FEDHA ZA SHULE MAKETE

Unknown | Tuesday, February 13, 2018 | 0 comments


Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Ihanga iliyopo kijiji cha Ihanga kata ya Ukwama Wilayani Makete Mkoani Njombe Mwl.Amos Mpandila kwa kushirikiana na Kamati ya shule hiyo chini ya Mwenyekiti wake Fedick Sanga wanatuhumiwa kutumia vibaya fedha za ujenzi wa choo cha wanafunzi kwa kubadilisha matumizi na kusababisha ujenzi huo kusimama na kuleta sintofahamu kubwa kwa Wananchi
Fedha hizo zaidi ya Milioni 4 zimetumika isivyo baada ya kutakiwa kujenga choo chenye mashimo manne badala yake ukafanyika ukarabati uliochini ya kiwango tofauti na Maelezo yaliyomo kwenye mwongozo wa ujenzi wa choo (BOQ)
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw.Fedenicko Ndelwa amesema fedha hizo zilitakiwa kununua mchanga kutoka Makambako lakini haujanunuliwa badala yake wanafunzi wakaagizwa kutafuta mchanga porini,tanki la maji lilitakiwa linunuliwe lenye ujazo wa Lita elfu 5 lakini limenunuliwa lenye ujazo wa Lita  elfu 2,bati halijanunuliwa hata moja zimetumika chakavu n.k
Kamati ya uchunguzi iliyoundwa na Mh.Diwani wa kata ya Ukwama Augustino Tweve ikabaini mapungufu mengi tu na kumlazimu Diwani huyo kuitisha mkutano na wananchi wa kijiji hicho uliotawaliwa na wananchi wenye jazba wakitaka kujua matumizi ya fedha hizo
Mwalimu mkuu alipoulizwa na kamati hiyo aliieleza kuwa"Samahani nakiri kosa kwa kutumia fedha zingine kununua miti ya parachichi na mbolea yake tofauti na mwongozo wa matumizi ya fedha hizo"
"Fedha zingine laki moja na elfu sitini nilitumia nauli kwenda Makete mjini kuchukua fedha kwa ajili ya ukarabati wa choo hiki kinyume na mwongozo"
Jambo ambalo wananchi walipingana nalo vikali kwa kukiuka taratibu na miongozo ya matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali
Kamati iliyoundwa ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mzee Michael Nundu iliendelea kusema"kamati ya shule imetukimbia kufanya uchunguzi na kushindwa kuwahoji wakimkimbia hata Mkuu wa shule waliyeshirikiana naye katika kupanga matumizi hayo kinyume"
Diwani alilazimika kuiagiza kamati ya shule ndani ya wiki moja ikae na kujadili jambo hilo ili kurudi kwa fedha za Serikali zilizotumika vibaya lakini Mwenyekiti wa kamati ya shule bw.Fedick Sanga akagomea kufanya hicho na kusema yupo tayari kwa lolote lakini hatotekeleza agizo hilo
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG