Home » » CHADEMA Yapata Pigo Tena....Ni Baada ya Mgombea Wake Kuhamia CCM Siku Tatu Baada ya Kuzindua Kampeni

CHADEMA Yapata Pigo Tena....Ni Baada ya Mgombea Wake Kuhamia CCM Siku Tatu Baada ya Kuzindua Kampeni

Unknown | Monday, February 05, 2018 | 0 comments
Chadema kimepata pigo baada ya mgombea wake wa udiwani Kata ya Manzase wilayani Chamwino Mkoa wa Dodoma, Mashaka Chalo kujiunga na CCM pamoja na wanachama wengine 131.

Chalo amehama Chadema siku ya tatu tangu chama hicho kikuu cha upinzani nchini kuzindua kampeni katika Kata hiyo na kunadiwa jukwaani na mbunge wa viti maalum, Kunti Majala.

Uchaguzi wa ubunge jimbo la Siha, Kinondoni na katika Kata 10 nchini utafanyika Februari 17, 2018. Uchaguzi katika Kata hiyo unafanyika baada ya aliyekuwa diwani, Peter Madanya (CCM), kufariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.

Mgombea huyo amehamia CCM  Februari 4, 2018 katika kijiji cha Manzase wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho na kupokewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rodrick Mpogolo.

Mbunge wa Mtera (CCM),  Livingstone Lusinde amesema uamuzi wa Chalo kujiuzulu ni ushindi kwa chama tawala.

“Mpogolo unaweza kufungua kampeni hizi na kisha kuzifunga maana kazi imekwisha. Tulikuwa na  wagombea watatu, lakini kuondoka kwa huyu,  CCM tunaona kazi imekwisha. Wagombea wengine waliobaki  hata tukilala usingizi hakuna kitu ushindi ni wetu,” amesema.

Mgombea wa CCM katika Kata hiyo ni Amosi Mloha.

Lusinde amesema Chadema walimpitisha Chalo dakika za mwisho kuwania udiwani bila kujua kuwa alikuwa pandikizi la CCM.

Akizungumza katika mkutano huo Chalo amesema amerejea CCM kwa sababu ni chama chake na kimemlea.

Advertisement
==

Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG