Home » » KAULI YA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA NJOMBE JASEL MWAMWALA ATOA TAMKO KUHUSU WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI

KAULI YA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA NJOMBE JASEL MWAMWALA ATOA TAMKO KUHUSU WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI

Unknown | Monday, January 08, 2018 | 0 comments



Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa njombe mh Jasery mwamwala amewaomba wazazi na walezi mkoa wa njombe kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama pale ambapo mtu anapatikana amempa ujauzito mwanafunzi na kukatiza ndoto zao.


Ameyasema hayo wakati akizungumza na kituo hiki mapema hii leo ambapo amesema kumekuwa na changamoto katika mkoa wa njombe ya wanafunzi kupata ujauzito wakati bado wanasoma na kukatiza ndoto zao za kujiendeleza kielimu.


Mwamwala ameongeza kuwa mikakati ya viongozi katika mkoa wa njombe ni kutaka mimba isiwepo mashuleni ili wanafunzi watimize ndoto zao pia amesema kwa wanaume wanao wapa mimba wanafunzi dawa yao inachemka na wataanza kushughulikiwa kisheria.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG