Home » » Lissu: "Walikuwa watu wawili, mmoja mwembamba niliona akishuka huku ameshika "Machine gun"

Lissu: "Walikuwa watu wawili, mmoja mwembamba niliona akishuka huku ameshika "Machine gun"

Unknown | Monday, December 11, 2017 | 0 comments
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kupitia CHADEMA amesema anaendelea vizuri  na atarejea nchini akiwa salama


Lissu ameyasema hayo leo mchana wakati akifanya mahojiano na idhaa ya Kiswahili ya Kijerumani (DW).
"Madaktari wangu wamenihakikishia kuwa nitarejea nchini na nitaendelea na shughuli zangu kama kawaida", amesema
Katika hatua nyingine Lissu amesema anachokumbuka katika tukio hilo wakati wanaingia getini kulikuwa na gari moja nyeupe limesimama huku kulikuwa na watu wawili.
"Walikuwa watu wawili, mmoja mwembamba niliona akishuka huku ameshika "Machine gun" baadaye najishtukia nipo hospitali Nairobi", ameongeza.
"Ninachoshangaa ndani ya ile nyumba kuna ulinzi mkali walikuwa wapi walinzi wakati nashambuliwa", amesema.
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG