Home » » Msiwachague Nyalandu, Mtulia na Molel wakigombea - Peneza

Msiwachague Nyalandu, Mtulia na Molel wakigombea - Peneza

Unknown | Friday, December 15, 2017 | 0 comments
Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA),  Upendo Peneza amefunguka na kuwataka wananchi mbalimbali kutowachagua baadhi ya Wabunge ambao wamejiuzulu nafasi zao za Ubunge kupitia vyama vyao vya siasa kama watakwenda kugombea tena kupitia vyama vingine

Upendo Peneza amesema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kusema yeye hafurahishwi na hama hama hizo zinazofanywa na Wabunge hao kwani zinaingiza nchi katika gharama kubwa ya uchaguzi wa marudio ambapo fedha hizo zingeweza kutumika kufanya maendeleo na kutatua changamoto zinazowakumba wananchi. 
"Wabunge wa majimbo kuhama kwenda chama kingine kwani unabadilika sura? Nawaomba Watanzania wenzangu na wananchi kiujumla kama hawa viongozi na hii hama hama inayoendelea watarudi kwa mgongo wa vyama vingine nawaombeni sana msiwachague kwa sababu gharama zinazotumika kwenye huo uchaguzi ni gharama ambayo ingekuletea hospitali, gharama ambayo ingeweza kununua taulo za kike watoto wakasoma shuleni vizuri" alisema Upendo Peneza 
Aidha Mbunge huyo amewashauri wabunge wengine wa majimbo ambao wanataka kuhama vyao vyao kuwa ni bora wasubiri na kuvumilia mpaka mwaka 2019 ambapo Katiba inawaruhusu ili uchaguzi wa marudio usifanyike na kuokoa fedha za Watanzania. 
"Pale ambapo Watanzania wameingia gharama kwa sababu yako, pale ambapo kodi zetu zimetumika kukuweka pale tusaidie tu mpaka baada ya miaka mitano ikishakwisha agana nao salama au vumilia mpaka 2019 ambapo Katiba itakuruhusu ukihama chama 2019 hatutakwenda kwenye uchaguzi mwingine tutavumilia mpaka 2020 kwa sababu kuna muda wa kurudia uchaguzi. Kwa hiyo nawashauri wale ambao wanataka kuunga mkono kwa kuhama wasubiri ule muda unaoruhusiwa Kikatiba na wahame kipindi hicho ampapo nchi haitaweza kuingia gharama yoyote ile kupata muwakilishi mpya" alisisitiza Upendo Peneza 
Mpaka sasa Wabunge wa majimbo matatu wametangaza kuhama vyama vyao na kupoteza sifa ya kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo majimbo yao yatakwenda kufanya uchaguzi wa marudio siku za usoni, wabunge hao ni pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Siha (CHADEMA) Dr.Godwin Mollel ambaye amehamia (CCM), aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini (CCM) Lazaro Nyalandu ambaye amehamia (CHADEMA) na aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni Dar es salaam, Maulid Mtulia kupitia Chama cha C.U.F ambaye amehamia (CCM).
Share this article :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Copyright © 2018. AFRICAN NEWS BLOG - All Rights Reserved
Imetengenezwa na Edwin Moshi
Inaendeshwa na AFRICAN NEWS BLOG